Mwaka 2014 umefika ukingoni. Ni mambo mengi sana yamefanyika katika huu mwaka. Katika upande wa teknolojia, tumeona hatua na maendeleo makubwa sana katika nyanja hii, ikumbukwe pia huu ndio mwaka ambao Internet imetimiza miaka 20. Tutaangazia mambo yaliyokuwa gumzo katika mwaka 2014 hasa katika teknolojia ya smartphones, tukigusa katika sehemu mbalimbali kukuwezesha wewe msomaji kutambua ni yapi hasa yaliyojiri na kuleta msisimko.
Uzinduzi wa HTC M8
Uzinduzi wa HTC M8
Mnamo mwezi March mwaka huu HTC alizindua flagship smartphone hii, ikiwa ni muendelezo wa mfululizo wa HTC One smartphones, ambapo ndio smartphone iliyopewa jina rasmi la HTC One. Toleo la nyuma(predecessor) wake ni HTC M7. Asilimia kubwa ya umbo lake la nje limetengenezwa kwa madini ya Aluminium. Ina maboresho na mabadiliko baadhi ukilinganisha na M7. M8 imetokea kupendwa na watumiaji wengi sana wa smartphones ikiwa na display ambayo ina muonekano murua kabisa ikitumia teknolojia ya Super LCD3 capacitive display katika kiwango cha pixel density ya


