Showing posts with label iphone6. Show all posts
Showing posts with label iphone6. Show all posts

Dec 31, 2014

Yaliyojiri Mwaka 2014 Katika Teknolojia Ya Smartdevices (1/2)

Mwaka 2014 umefika ukingoni. Ni mambo mengi sana yamefanyika katika huu mwaka. Katika upande wa teknolojia, tumeona hatua na maendeleo makubwa sana katika nyanja hii, ikumbukwe pia huu ndio mwaka ambao Internet imetimiza miaka 20. Tutaangazia mambo yaliyokuwa gumzo katika mwaka 2014 hasa katika teknolojia ya smartphones, tukigusa katika sehemu mbalimbali kukuwezesha wewe msomaji kutambua ni yapi hasa yaliyojiri na kuleta msisimko.


Uzinduzi wa HTC M8
Mnamo mwezi March mwaka huu HTC alizindua flagship smartphone hii, ikiwa ni muendelezo wa mfululizo wa HTC One smartphones, ambapo ndio smartphone iliyopewa jina rasmi la HTC One. Toleo la nyuma(predecessor) wake ni HTC M7. Asilimia kubwa ya umbo lake la nje limetengenezwa kwa madini ya Aluminium. Ina maboresho na mabadiliko baadhi ukilinganisha na M7. M8 imetokea kupendwa na watumiaji wengi sana wa smartphones ikiwa na display ambayo ina muonekano murua kabisa ikitumia teknolojia ya Super LCD3 capacitive display katika kiwango cha pixel density ya

Oct 5, 2014

BlackBerry Passport versus iPhone 6 plus; Kazi versus Starehe.

Mwezi jana, yaani Septemba umekuwa bize sana katika ulimwengu wa teknolojia, hasa ya smartphones. Apple alizindua model nyingine ya iPhone zikiwa ni model mbili, iPhone 6 na iPhone 6 plus. Pia alizindua smartwatch. BlackBerry hajafa, anadunda kama kawaida na hakusita kuleta flagship nyingine katika mwezi huohuo wa Septemba, BlackBerry Passport! ndivyo inavyojulikana. Huawei pia alizindua simu zake za line ya Ascend Mate, sitamzungumzia sana kwa sababu si mhusika katika makala hii.

iPhone 6 plus

Linapokuja swala la kuchagua simu ipi ni bora zaidi ya nyingine au simu ipi inafaa zaidi kununua, specifications si jambo pekee linaloweza kukupa suluhisho la utata huu. Mtindo wa maisha(lifestyle) ni moja ya swala la kuzingatia katika kujua ni simu ipi inakufaa. Hii ina maana kubwa sana! iPhone 6 plus na BlackBerry Passport
zote ni smartphones tena za hali ya

Sep 10, 2014

Most of us are dissapointed.

"Wengi wetu tumesikitishwa", hivyo ndivyo kichwa cha habari kinavyosema. Siku chache zilizopita niliandika makala kuhusu ni vipi na kwanini iPhone 6 itaweza badili muonekano wa teknolojia ya smartphone. Bahati mbaya sana hili limekuwa tofauti, vitu vingi tulivyotegemea kuviona katika simu hizi mbili za iPhone 6 hatujaviona! iPhone 6 4.7 inch inakatisha tamaa kabisa, battery yake ni karibia na ileile iliyopo katika iPhone 5S. Pixel density ni ile ile ya iPhone 5S hadi iPhone 4, hakuna tofauti kubwa sana katika smartphone hii zaidi ya kuwa na display ya ukubwa wa 4.7inch, processor yenye uwezo zaidi na mengine baadhi. Hakuna display ya Sapphire katika model zote mbili, wametumia Gorilla Glass ambayo wanatumia tangu kuanzishwa kwa iPhone. Labda kwa iPhone 6 plus, angalau kuna vitu vya kuvutia. Display yake ni Full High Definition(HD), 1080p resolution. Camera ina Optical Image Stabilisation(OIS) na pixel density yake ina kiasi cha 401ppi(pixel density per inch). Uwezo wake wa battery ni mkubwa kuliko iPhone 6 4.7 inch.



Sep 4, 2014

iPhone 6! pengine itakuwa smartphone bora kuwahi kutengenezwa katika historia.

Ni takribani miaka 16 tangu neno "smartphone" kuanza kutumika, aina hii ya simu ina historia ndefu sana ambapo inarudi hadi miaka ya 1970. Umaarufu wake haswa umekuja mnamo mwaka 1998 ambapo kampuni ya Ericsson ilizindua simu inayoitwa Penelope na hapo ndipo neno smartphone likachipuka. Simu hii ilikuwa na uwezo ambao pengine unaweza kusema ni sawa na ule wa kompyuta. Baada ya hapo makampuni mengine mengi nayo yalianza kutengeneza smartphones, mfano BlackBerry, Nokia, Palm, Dell, HP na kadhalika. Miaka imesonga na tumeona mabadiliko mengi sana katika fani hii ya teknolojia, makampuni yanayotengeneza smartphones ni mengi sana kwa sasa, Operating Systems za simu hizi nazo zipo nyingi, watumiaji wa simu hizi nao wanaongezeka kila siku. Karibia kila mtu anamiliki simu hii.
iPhone 6 upande wa kulia ikiwa na iPhone 5S.