Jan 3, 2014

Nokia hajakata tamaa na mpango wake wa smartphone ya Android.

Pengine Lumia zitumiazo Android zitakuwa na muonekano huu.
Inaonekana wazi Nokia hajatupilia mbali mpango wake wa kuwa na smartphone itayotumia Android. Mwishoni mwa mwaka jana wa 2013 tetesi zilivuja mtandaoni zikionesha simu ya Nokia iitwayo Normandy ambayo inasemekana inatumia Android OS lakini ikiwa na misingi ya smartphone za Nokia Asha s40. Baada ya muda mfupi Nokia walikanusha taarifa hizo,tunajua hizi ni blahblah tu. Nokia hataki kusema wazi mipango yake,inasemekana mpango huu unapigwa chinichini na pia tusitegemee kuona smartphone hizi katika siku za usoni,itachukua muda kidogo mpaka kuingizwa sokoni.


Pamoja na Nokia kununuliwa na Microsoft lakini pia hafungwi kuweza kufanya miradi mingine ambayo haihusiani na Microsoft.Windows Phone OS inakua kwa kasi sasa na umaarufu wa simu za Nokia Lumia unaongezeka kutokana na kuwa na kamera zenye kutoa picha zenye ubora wa hali ya juu,lakini pamoja na sifa zote hizi watu wanataka kuona Lumia zikitumia Android,kamera tu haitoshi kumvuta mtu kununua simu bali operating system ndicho kilicho cha msingi zaidi.Kwa upande wangu nadhani Nokia anatakiwa pia kutumia Android OS hii itamuongezea umaarufu katika soko kwa sababu watu wengi wenye mapenzi na Nokia wanataka kuziona zikitumia Android OS.

No comments :

Post a Comment