![]() |
Alicia Keys katika uzinduzi wa smartphone za BB1O |
Alicia Keys anaondoka BlackBerry huku akiwa na doa katika nafasi aliyokuwa akishikilia.Hapo mwanzo wakati anaanza kazi yake ya kuzitangaza smartphones za BlackBerry 10 aliwahi kutweet katika mtandao wa Twitter kwa kutumia iPhone na wakati alitakiwa kutumia BlackBerry Z10,smartphone ambayo alikuwa akiitangaza,swala hili lilizua mzozo sana.Alijitetea kwa kudai kwamba akaunti yake ilikuwa hacked. na si yeye aliyetweet.
Msemaji wa kampuni ya BlackBerry alisema kwamba"tumemaliza ubia wetu wa mwaka mmoja na Alicia Keys".Hakusema zaidi kwamba ni sababu gani iliyosababisha kuondoka kwa msanii huyu.Nadhani nyimbo yake haitakiwi kuitwa "Thi Girl Is On Fire" bali "This Girl Has Been Fired",usitilie maanani!ni utani tu!
No comments :
Post a Comment