Miaka 11 iliyopita Nokia alizindua smartphone hii, enzi hizo Nokia 6600 ilikuwa ndiyo smartphone yenye kutumia teknolojia ya hali ya juu katika smartphones zote za Nokia zilizowahi kutengenezwa kabla. Ikiwa na camera, TFT(Thin Film Transistor) display yenye uwezo wa rangi 65,000(65k), uwezo wa kucheza muziki na display yenye muonekano wenye kiwango cha hali ya juu. Smartphone nyingi zilizokuwepo kipindi hicho hazikuwa na uwezo kama huu. Ili kuweza kuimiliki smartphone hii kwa muda huo ilibidi uwe na shilingi za kitanzania zipatazo laki tisa, unaweza fikiria kwa mwaka 2003 shilingi laki tisa ilikuwa na thamani kiasi gani kulinganisha na thamani ya pesa kwa sasa.
 |
| Nokia 6600 |
Miaka hiyo hakukuwepo smartphone zenye processors kama zilizopo sasa mfano. dual core processors(CPU mbili), quad core processor(CPU nne) n.k ambazo nyingi ya hizi huwa na spidi inayoanzia 1.5GHz(Giga-Hertz) na kuendelea kwa kila CPU. Single core(CPU moja) processor ndizo zilikuwa zikitumika, Nokia 6600 ikiwa na processor ya single core yenye spidi(clock speed) ya 104MHz(Mega-Hertz), ni processor yenye spidi ndogo sana ukilinganisha na teknolojia tuliyonayo sasa, lakini kwa muda huo processor hii ilikuwa ikionekana yenye