Showing posts with label urithi. Show all posts
Showing posts with label urithi. Show all posts

Dec 30, 2014

Nokia 1100, inaongoza kwa mauzo duniani katika historia ya simu za mkononi.

Nokia tochi, kitochi, simu ya nyongeza, jiwe; Haya ni baadhi ya majina aliyobatizwa Nokia 1100. Simu hii ni maarufu sana na sidhani kama kuna mtu ambaye hajawahi kuiona machoni mwake. Ilikuwa ikipendwa na watumiaji wengi kutokana na uimara iliyokuwa nao, uwezo maradufu wa kukaa na chaji, na unafuu wa bei yake.
Nokia 1100

Siku hizi tumezoea kuona smartphones kila mahali, maisha yetu yamezungukwa na matumizi makubwa ya smartphones katika kuchat, kuperuzi mtandao, kupiga picha, kusoma vitabu na mengine mengi. Kila mara smartphones mpya hutoka. Leo utasikia HTC One M8, mara kesho iPhone 6 Plus, ukiamka kesho kutwa Samsung Galaxy Note 4 iko sokoni. Lakini pamoja na uzinduzi huu wote na hekaheka za mauzo na manunuzi ya smartphones. Hakuna smartphone yoyote iliyowahi kufikia hata nusu ya

Dec 14, 2014

Nokia 6600, moja ya urithi muhimu sana katika historia ya smartphones.

Miaka 11 iliyopita Nokia alizindua smartphone hii, enzi hizo Nokia 6600 ilikuwa ndiyo smartphone yenye kutumia teknolojia ya hali ya juu katika smartphones zote za Nokia zilizowahi kutengenezwa kabla. Ikiwa na camera, TFT(Thin Film Transistor) display yenye uwezo wa rangi 65,000(65k), uwezo wa kucheza muziki na display yenye muonekano wenye kiwango cha hali ya juu. Smartphone nyingi zilizokuwepo kipindi hicho hazikuwa na uwezo kama huu. Ili kuweza kuimiliki smartphone hii kwa muda huo ilibidi uwe na shilingi za kitanzania zipatazo laki tisa, unaweza fikiria kwa mwaka 2003 shilingi laki tisa ilikuwa na thamani kiasi gani kulinganisha na thamani ya pesa kwa sasa.

Nokia 6600

Miaka hiyo hakukuwepo smartphone zenye processors kama zilizopo sasa mfano. dual core processors(CPU mbili), quad core processor(CPU nne) n.k ambazo nyingi ya hizi huwa na spidi inayoanzia 1.5GHz(Giga-Hertz) na kuendelea kwa kila CPU. Single core(CPU moja) processor ndizo zilikuwa zikitumika, Nokia 6600 ikiwa na processor ya single core yenye spidi(clock speed) ya 104MHz(Mega-Hertz), ni processor yenye spidi ndogo sana ukilinganisha na teknolojia tuliyonayo sasa, lakini kwa muda huo processor hii ilikuwa ikionekana yenye