Dec 8, 2013

Samsung anafanyia majaribio baadhi ya simu za kati(midrange smartphones) kama zitaweza tumia Android 4.4 KitKat.

Samsung anafanyia majaribio baadhi ya simu za kiwango cha kati(midrange) kama zinaweza kutumia Android 4.4 KitKat bila shida.Listi ya simu hizo imevuja mtandaoni na imetaja simu zifuatazo.

  • Samsung Galaxy S3 Mini
  • Samsung Galaxy S4 Mini
  • Samsung Galaxy Ace 2
  • Samsung Galaxy Fame
  • Samsung Galaxy Core
  • Samsung Galaxy Ace Advance
Kama unakumbuka hapo mwanzo wakati Android version hii inakaribia kuzinduliwa Google alisema ya kwamba version hii itaweza kufanya kazi katika simu zenye uwezo mdogo kabisa(low end) zenye hadi RAM ya uwezo wa 512MB.
Endapo majaribio ya KitKat yatafanikiwa katika simu hizi basi watumiaji wake wataweza pata official update hapo mwakani baadaye.Hii inatokana na kwamba mpaka simu zote za hali juu(high end) zipate update ndipo midrange zitafuata.

No comments :

Post a Comment