Oct 22, 2013

Utoaji wa app ya BBM kwenye Android na iOS umerudi tena.

Jana asubuhi kampuni ya BlackBerry ilitangaza kwamba inaanza kutoa tena app ya BBM kama ilivyoahidi wiki kama nne zilizopita baada ya kuwa na tatizo katika uzinduzi wake lililopelekea kusimamishwa kwa kuendelea kutoa app hii,hali hii ilitokana na watu wengi kuwa na app feki kitu kilichopelekea msongamamo wa mawasiliano kwenye server ya BlackBerry.


Kwa sasa wataoweza kutumia app hii ni wale waliojisajili mapema kwenye tovuti ya bbm.com,wale ambao wamechelewa kujisajili itabidi wasubiri mpaka watapotumiwa email ya kukubaliwa kutumia app hii.

Kwa sasa inapatikana katika Android katika simu za Samsung Galaxy zinazorun Android 4.0 na kuendelea katika store ya Samsung apps.

 Kama tayari umeanza tumia app hii kwenye Android au iOS,share nasi unaionaje.


No comments :

Post a Comment