May 21, 2013

Windows Phone inakua haraka kuliko Android na iOS,imesema ripoti ya hivi karibuni.


Katika miezi ya karibuni tumeona msukumo mkubwa sana kwa Windows Phone.Ripoti iliyotolewa na Kantar World Panel imeonesha ukuaji katika miezi mitatu iliyopita.Windows Phone imekua kwa 1.5% kutoka Februari mpaka Machi,iOS imekua kwa 0.2% na Android imeporomoka kwa 1.9%.Kuanzia mwaka jana muda kama huu Windows Phone imekua kwa 3.7%.Nokia pekee imekua kwa asilimia kutoka 1% mpaka 4% katika hisa sokoni katika mwaka mmoja.


Sababu ya ukuaji huu imetokana na watuniaji wa simu zisizo smartphones(feature phones).52% ya wale waliohamia kutumia Windows Phone walikuwa watumiaji wa simu za kawaida(feature phones).Hicho ni kiasi kikubwa zaidi ya watumiaji wa Android na iOS.Inamaanisha watu ambao hawajawahi kutumia smartphones walivutiwa na kutumia simu za Windows.Hiki ni kitu kizuri na kwa sasa inashikilia na nafasi ya tatu baada ya Android na iOS.

No comments :

Post a Comment