Ikiwa wewe ni mfuatilia wa blogu hii kwa hakika hii haitakuwa mara yako ya kwanza kukutana na makala inayohusiana na kuroot smartphone za Android. Lakini ikiwa wewe ni mpya katika blogu hii au ungependa kujua zaidi nini maana ya rooting katika Android na inafanya nini hasa, unaweza kusoma makala yetu iliyotangulia "Nini maana ya Rooting katika Android OS" HAPA. Hapo awali tulishaandika njia mojawapo ya kuroot smartphone za Android kwa kutumia app ya towelroot, pia unaweza soma makala nzima "Njia rahisi kabisa ya kuroot smartphone ya Android OS" HAPA.
Makala hii inakuletea njia nyingine ya kuroot smartphone yako ya Android kirahisi kwa kutumia app inayoitwa Kingo ROOT. Unaweza kuroot kwa kutumia app hii kwa njia mbili, kwa kupitia PC au kwa njia ya moja kwa moja bila kutumia PC. Njia hizo mbili zinaelezewa hapa chini;