Showing posts with label rooting. Show all posts
Showing posts with label rooting. Show all posts

Jul 7, 2015

Na Hii Ndiyo Njia Nyingine Rahisi Ya Kuroot Android Yako

Ikiwa wewe ni mfuatilia wa blogu hii kwa hakika hii haitakuwa mara yako ya kwanza kukutana na makala inayohusiana na kuroot smartphone za Android. Lakini ikiwa wewe ni mpya katika blogu hii au ungependa kujua zaidi nini maana ya rooting katika Android na inafanya nini hasa, unaweza kusoma makala yetu iliyotangulia "Nini maana ya Rooting katika Android OSHAPA. Hapo awali tulishaandika njia mojawapo ya kuroot smartphone za Android kwa kutumia app ya towelroot, pia unaweza soma makala nzima "Njia rahisi kabisa ya kuroot smartphone ya Android OSHAPA.

Makala hii inakuletea njia nyingine ya kuroot smartphone yako ya Android kirahisi kwa kutumia app inayoitwa Kingo ROOT. Unaweza kuroot kwa kutumia app hii kwa njia mbili, kwa kupitia PC au kwa njia ya moja kwa moja bila kutumia PC. Njia hizo mbili zinaelezewa hapa chini;

Jun 23, 2015

Njia rahisi kabisa ya kuroot smartphone ya Android OS.

Kipindi cha nyuma nilishawahi kuelezea katika blogu hii maana ya rooting. Katika operating system ya Android, rooting ni mchakato wa kufungua mfumo(system) wa Android ili kuweza kupata uwezo zaidi wa kuitawala smartphone yako. Operating system huwa na makabrasha(files and folders) ambayo huwezi pata uwezo wa kuyafanya chochote mpaka utapofanya mchakato wa rooting.

Unaporoot smartphone ya Android tunasema kwamba umepata "system privileges" ikimaanisha kwamba una vipaumbele vya kuweza kuitawala operating system ya simu yako. Hii itakuwezesha kufuta apps zilizopo katika system, kuzifanya apps unazodownload katika playstore kuwa apps za system(changing application softwares into system softwares), kubadili maandishi(fonts), kuweka operating systems zisizo rasmi(custom roms) na mengineyo mengi.

Kuna njia ambazo hutumika ili kuwezesha rooting kukamilika. Unaweza tumia programu za kompyuta au programu(apps) za Android, inategemea na njia unayochagua kutumia. Kuna baadhi ya njia ambazo hupunguza ugumu wa mchakato huu. Nitaelezea njia moja ambayo kwa sasa ni rahisi sana na inakubali katika smartphone za aina nyingi mno kuanzia Huawei mpaka HTC.

Njia hii hutumia programu(app) ambayo utaidownload na kuinstall katika smartphone yako, app inafahamika kama Towelroot. Kwa kutumia app hii, rooting ni mchakato wa dakika moja tu!. Nitaeleza hatua za mchakato huu. 

Dec 28, 2013

Nini maana ya Rooting katika Android OS.

Mtengeneza simu yoyote anapoitengeneza simu yake huweka mipaka ambayo yule mtumiaji anapoitumia bidhaa hiyo hawezi kuivuka mipaka hiyo kwa hali ya kawaida.Pia hata mitandao ya simu mfano.Vodacom,Airtel inapouza simu hasa smartphones(ambazo zinatumia sim card za mitandao yao tu) huweka apps zao ambazo kwa hali ya kawaida huwezi kuzifuta wala kuzirekebisha.Hapa ndipo mfumo wa kufanya rooting ulipotokea ili kuweza kutatua hili tatizo.

Rooting ni mchakato wa kuifanya smartphone ya Android kuweza kufikiwa mpaka pale ambapo mtengeneza simu hiyo ameweka mipaka.Hii ina maana kwamba rooting inakupa uwezo wa kufuta apps ambazo zimekuja na simu(pre-installed apps),kuweza kubadilisha au kuboresha operating system nzima ya simu,kuweza kurekebisha source code ili kuweza kubadili baadhi ya commands katika operating system na mambo mengine kadhalika.

Android OS imetengenezwa kwa msingi wa operating system ya kompyuta inayoitwa Linux OS.Inatumia Kernel(ni programu ambayo kazi yake ni kufanya michakato ya taarifa zinazotoka na kuingia katika programu nyingine katika kompyuta,hutafsiri taarifa zote za programu mbalimbali katika CPU ya kompyuta) ya Linux.

Unapofanya rooting unakuwa umeingia ndani ya operating system ya Android na kuweza kufanya lolote lile.Hii inapelekea simu husika kuwa katika usalama mdogo hasa katika kushambuliwa na programu hatari(malicious softwares) ambazo zinaweza kuchukua taarifa kutoka katika simu bila ruhusa ya mmiliki.