May 26, 2013

Sababu kumi zinazoweza sababisha Android kumuua iOS.

1.ANDROID INAPATIKANA KATIKA SIMU ZAIDI YA MOJA-kama ni mtumiaji wa Android unakuwa na machaguo mengi ya makampuni yanayotengeneza simu za Android unaweza tumia Samsung,LG,Alcatel,Sony na nyinginezo nyingi lakini ni tofauti na iOS ambapo inapatikana katika simu moja tu ya iPhone wanayotengeneza wenyewe,kwa hili  unajikuta una mipaka ya kuchagua brands.

 2.APPLE WANATENGENEZA SIMU ZA GHARAMA TU(high-end devices)-Kama unapenda simu ya Apple na unataka simu ya bei nafuu huwezi kupata sababu zote ni simu za gharama.Tofauti na Android ambapo kuna smartphones za bei nafuu hadi laki moja.

 3.ANDROID KUIBADILI MUONEKANO WAKE KADIRI UNAVYOTAKA(Customisation)-Unaweza kubadili muonekano wa Android kirahisi,mfano.kuweka custom rom ambapo huwezi fanya hiki kitu katika simu za iPhone.

4.GOOGLE PLAYSTORE YA ANDROID INA APP NYINGI NZURI ZA BURE TOFAUTI NA APP STORE YA iOS-Unapata application nyingi sana nzuri katika Android bure tofauti na iOS ambapo apps nyingi nzuri ni za kulipia.

5.ANDROID INA MUONEKANO MZURI NA FEATURES NYINGI KWA APPS ZINAZOTENGENEZWA NA GOOGLE KAMA GOOGLE+,GOOGLE MAP,YOUTUBE,GMAIL NA NYINGINEZO.
6.WIDGETS-hivi ni vidirisha vidogo ambavyo huonesha application inavyoendelea kwa kukupa updates ambapo vinapatikana katika Android na iOS hana feature kama hii.

7.iPHONE HAZINA SEHEMU YA KUWEKEA MEMORY CARD-Simu za Apple iPhone hazina sehemu ya kuwekea memory card(sd card slot) ambapo simu nyingi za Android zina card slot kwa hiyo inakuwa rahisi kuonegeza ukubwa ukubwa wa memory.

 8.NI RAHISI KUSHARE DATA KATIKA ANDROID- Kwa kutumia NFC na Android Beam ni rahisi kuhamisha data kutoka device moja kwenda nyingine kwa kubonyeza mara moja.

 9.ANDROID NI RAHISI KUTUMIA-Kwa mtu ambaye hajawahi kutumia smartphone kabla na hata mtumiaji mwingine ataona kuna ugumu katika kutumia iPhone kuliko kutumia Android.

 10.ANDROID INAKU HARAKA KULIKO iOS-Kila siku watumiaji wengi wapya wananunua simu za Android kuliko iOS.

No comments :

Post a Comment