May 14, 2013

BlackBerry Messenger(BBM) inakuja katika android na iOS

Kampuni ya kutengeneza smartphone ya Research In Motion inayotengeneza simu aina ya blackberry imeamua kuifanya software yake maarufu kama BBM kuwa cross-platform application(yaani inayopatikana katika OS zaidi ya moja) kama zilivyo social apps nyingine kama Viber na Whatsapp. BBM imekuwa moja katika ya application maarufu sana katika simu za BlackBerry,CEO wa RIM Mr. Thorstein Heins ametangaza katika kiangazi kinachokuja kwa majira ya marekani BlackBerry messanging itapatikana kama thrid party app katika mobile operating system maarufu kama iOS na android.Kwa sasa,BBM ina features kama chats,kutumiana picha,sauti na video na vinginevyo. Thorstein amesema itakuja na maboresho makubwa kama video calling,kushare screen na vinginevyo ambavyo kwa sasa vinapatikana katika operating system ya bb10 ambayo inapatikana katika simu kama blackberry z10 na q10.Itapatikana katika ios zinazotumia ios 6.0 na kuendelea na kwa android kuanzia ice cream sandwich na kuendelea.Kwa hiyo,kuwa makini unaponunua simu ya iphone au android ili usije kosa bbm integration katika simu yako

No comments :

Post a Comment