May 14, 2013

Asilimia 74.4% ya simu katika robo ya kwanza ya mwaka 2013 zinatumia android,iOS ikiachwa nyuma tena kidogo

Kampuni ya moja ya takwimu iitwayo Gatner imetoa ripoti ikieleza mauzo ya simu katika robo ya kwanza ya mwaka 2013,Android ikiwa inaongoza operating systems nyingine

Katika smartphones 210 milioni zilizouzwa katika miezi mitatu ya mwanzo ya  mwaka huu,156 milioni zinatumia android.Huo ni muongezeko wa juu wa asilimia 17.5 ukiangalia kipindi kama hiki kwa mwaka jana.


Research in motion watengenezaji wa BlackBerry ni wa tatu wakiwa wameuza simu zipatazo 6.2 milioni,wakati microsoft ikiwa ikishusha pumzi kwa mauzo ya 6 milioni katika opearting system yake mpya. Samsung anaendelea kuwa namba moja katika watengeneza smartphones na anashikilia asilimia 30% ya mauzo yote,Kampuni ya Korea Kusini imeuza simu 64.7 milioni.Hiyo ni mara mbili ya simu kampuni ya Apple walizouza,wakiwa na mauzo ya asilimia 18.2% na kuuza simu 38.3 milioni.Unaweza kuona makampuni mengine katika chati hapo chini. Jumla ya mauzo ya simu kwa kampuni zote ni 425 milioni,ikiwa ni ukuaji wa ailimia 0.7% tu ukilinganisha na mwaka jana.Kiukweli gap kati ya Nokia na Samsung limeongezeka ukilinganisha na mwaka jana tofauti ilipokuwa 6 milioni tu lakini sasa ni karibu 37 milioni,hii inaifanya Samsung kuwa mbali sana.

No comments :

Post a Comment